News in Kiswahili

Ruto avunja kimya chake
Written by Grace Mburu   
Saturday, 14 August 2010 19:04

 

Siku mojaWakiongozwa na  waziri  wa elimu   ya  juu william ruto, wabunge hao wameelezea matumaini  yao kuwa,  serikali  itatimiza ahadi yake ya  kufanyia katiba mpya  marekebisho. Aidha  wanasema kuwa, kiu  yao  kuu  ni kuwaona vinara  wawili  serikalini, waziri  mkuu  , Raila Odinga  na Rais Mwai Kibaki  wakitimiza ahadi  walizotoa wakati wa  kampeni kuhusu katiba .  Viongozi  hao w a 'La' wlaikuwa wakizungumza walipoandaa karamu kwa wafuasi wao  katika bustani ya arboretum humu  jijini Nairobi. 

 

Ruto  amesema kuwa, anaunga mkono  kikamilifu utekelezaji  wa katiba , Iwapo tu itafanyiwa marekebisho   na kuwa, na manufaa  zaidi kwa  wananchi.    Anasisistiza kuwa, ni  sharti maslahi  ya  wakenya milioni  2.7  waliopinga katiba yashughulikiwa  haraka iwezekanavyo.   Ruto  pia  amepuuzilia mbali  vitisho vinavyotolewa  na wabunge kutoka chama cha ODM   vya  kumsimamisha  kazi kama  waziri,  sawia   na wenzake  serikalini  waliokuwa wakipinga katiba  mpya.   Ruto amesema kuwa,  uugwana  ni  kujadili  maswala   wala siyo kujadili watu binafsi .    mnamo  siku ya alhamisi,   katibu  mkuu  w a ODM, Nyang' Nyong'o  alisema kuwa, hatua kali zitachukuliwa dhidi ya  wafuasi  wa  ODM  waliopinga  katiba mpya.  Duru  zinaarifu  kuwa,rais Mwai  Kibaki na Waziri  mkuu Raila Odinga  ameitisha  kikao na  wabunge  , kitakacho =fanyika mnamo  siku  ya jumatatu kuzima  uwezekano  wa  tofauti  kali ambazo  huenda zikaibuka   pindi  bunge  litakapo  buni  kaamati maalum itakayoongoza utekelezaji  wa  katiba.   

 

 

Comments (0)
 


Capital Talk

You must have Flash Player installed in order to see this player.
Banner

Find us on...

extra xanax with marijuana online pharmacies tramadol